Rais Embalo: Jaribio la mapinduzi Guinea- Bissau limefeli; serikali inaendesha nchi


Rais Umaro Sissoco wa Guinea- Bissau jana usiku alitangaza kufeli na kugonga mwamba jaribio la mapinduzi nchini humo.

Njama hiyo ya kutaka kuipindua serikali ya Guinea-Bissau imejiri wakati baraza la mawaziri wa nchi hiyo likifanya kikao cha dharura na Rais na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Nuno Gomes Nabiam. Rais Umaro Sissoco Embalo wa Guinea-Bissau ameeleza kuwa jaribio la mapinduzi lililokusudiwa kumuondoa madarakani lilifeli jana Jumanne na amewatolea wito wananchi kote nchini kuwa watulivu. 

Akihutubiai taifa, Rais wa Guinea-Bissau ameeleza kuwa na hapa ninamnukuu" sikuwahi kufikiria kwamba kuna siku tutakumbwa na hali kama hii. Sikuwahi kudhania kwamba Waguinea-Bissau wanaweza kutekeleza kitendo kingine cha uibuaji machafuko," mwisho wa kunukuu 

Rais Embalo wa Guinea-Bissau ameongeza kuwa, vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo vilifyatuliana risasi na wahusika wa jaribio la mapinduzi lililofeli kwa muda wa masaa matano kabla ya kusambaratisha njama hiyo. 

Guinea Bissau baada ya jaribio la mapinduzi kufeli 
Ameongeza kuwa wanajeshi wengi walinda usalama wameuawa katika jaribio hilo la mapinduzi  na watu kadhaa wametiwa nguvuni hadi sasa kufuatia jaribio hilo la mapinduzi  lililofeli hata hivyo hakuweza kuthibitisha idadi kamili ya askari hao waliopoteza maisha. 

Rais wa Guinea-Bissau amesema ,anaamini kuwa wahalifu katika njama hiyo walikusudia kumuuwa yeye  na  mawaziri wengine wa serikali yake ambao walikuwa katika kikao chao cha kila wiki ikulu. 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments