Sakata la wabunge 19 wa Chadema laibuka tena

Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amesema wabunge 19 wa Viti Maalum wa Chadema waliopo bungeni wapo kihalali.

Hata hivyo amesema anasubiri michakato halali ndani ya chama chao na ngazi zingine ikithibitika hakuna shida atatekekeza takwa la kikatiba.

Novemba 2020 waliapishwa wabunge 19 wa Chadema ambao walizusha malumbano ya namna waliteuliwa na majina yao kupelekwa Bungeni kwani chama chao hakikutoa ridhaa.

Spika Dk Tulia ametoa kauli hiyo leo Jumatatu februari 14, 2022 jijini Dodoma wakati akizungumza na Wahariri na waandishi wa habari wanaoripoti Bunge.

Akijibu swali kuhusu uhalali wa wabunge wao, Spika amesema hadi sasa wabunge hao wapo kwa mujibu wa sheria kwani kila mbunge ni lazima atokane na chama na hao nao wametokana na chama.

Amesema Bunge halioni shida kuwaondoa wabunge na lilishawahi kufanya hivyo katika mabunge yaliyotangulia.

Hata hivyo amesema mchakato wa namna gani walifika Bungeni siyo hoja ambayo Bunge linatakiwa kujibu bali wenye majibu ni tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Dk Tulia amesema taarifa itakayopelekwa bungeni kuhusiana na wabunge hao sharti iwe imekidhi vigezo vyote vinavyotakiwa kwa kutendewa haki na yeye hatakuwa na shida kwenye maamuzi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments