Viwango elekezi vya kubadilisha fedha za kigeni leo Februari 17, 2022

 FRANKA ya Burundi inanunuliwa kwa shilingi 2.19 na kuuzwa kwa shilingi 2.206 huku dola ya Marekani nchini ikinunuliwa kwa Shilingi 2286.7525 huku ikiuzwa kwa Shilingi 2309.62.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya viwango elekezi vya kubadilisha fedha za kigeni iliyotolewa leo Februari 17, 2022 na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Wakati huo huo, Euro ya Ulaya inanunuliwa kwa shilingi 2599.81 na kuuzwa kwa shilingi 2626.04.

Aidha,kwa mujibu wa BoT, Paundi ya Uingereza inanunuliwa kwa Shilingi 3097.635 huku ikiuzwa kwa Shilingi 3129.535.

Yuan ya China inanunuliwa kwa shilingi 360.9 huku ikiuzwa kwa shilingi 364.03 na Yen ya Japan inanunuliwa kwa shilingi 19.8 na kuuzwa kwa shilingi 19.96.
Kwa upande wa Franka ya Rwanda inanunuliwa kwa shilingi 2.18 na kuuzwa kwa shilingi 2.24 huku shilingi ya Uganda ikinunuliwa kwa shilingi 0.62 na kuuzwa kwa shilingi 0.65.

Aidha, Randi ya Afrika Kusini inanunuliwa kwa shilingi 151.22 na kuuzwa kwa shilingi 152.58 huku shilingi ya Kenya ikinunuliwa kwa shilingi 20.14 na kuuzwa kwa shilingi 20.30.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments