WAJANE WA FAMILIA MOJA WAKABIDHIWA NYUMBA, SHILOLE, GLADY WAFUNGUKA "INAUMIZA"

      

Taasisi ya Glady Welfare imekabidhi Nyumba kwa Wajane watatu waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya makazi, Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Katika hafla hiyo, ambayo geni rasmi ni Mwanamuziki na Mfanyabiashara, Shilole maarufu kama Shishi Baby/ Shishi Food amezindua na kuwakabidhi nyumba Wajane hao ambao awali walikuwa wakiishi katika Kibanda cha Udongo akiwemo mmoja ambaye ni Mlemavu wa Macho.

Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Bi.Gladness Lyamuya amesema nyumba hiyo imejengwa kwa ufadhili wa Original East na michango ya Watu mbalimbali kupitia mitandao baada ya kuona ugumu wa maisha unaowakabili wajane hao, ambao wote ni Ndugu.

Amesema kuwa mbali ya kukabidhi nyumba hiyo, pia wametoa kiasi cha Shilingi Milioni 1 kama mtaji wa kibiashara.

"Huu ni muendelezo wa kusaidia, kama Taasisi hatuwezi kuwaacha hivi hivi lazima tuwape na mtaji, msaada huu tumeutoa kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali kupitia Instagram na Shirika la Original East ," amesema Mkurugenzi Glady.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments