YANGA SC YASONGA MBELE KOMBE LA ASFC, YAICHAPA BIASHARA UTD MABAO 2-1

 


KLABU ya Yanga imefanikiwa kutinga hatua inayofuata kwenye michuano ya Azam Sport Federation Cup (ASFC) baada ya kuichapa timu ya Biashara United kwa mabao 2-1 kwenye dimba la Benjamini Mkapa.

Yanga Sc ilianza kupata bao la kuongoza kupitia kwa beki raia wa DR Congo Yannick Bangala kwa bao zuri lililopeleka shangwe kwa mashabiki wa timu hiyo mnamo dakika ya 22 ya mchezo.

Bao la pili la Yanga Sc lilipatikana kwa dakika ya 28 ya mcheezo kwa mshambuliaji wao Fiston Mayele kabla ya Biashara United kupata bao la kufutia machozi kupitia kwa Opare dakika ya 38 kipindi cha kwanza.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments