Dk Mwigulu aiomba USAID dola 1.3 bilioni za Azaki

Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba ameliomba Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) kutoa dola bilioni 1.3 zilizokuwa zitolewe kwa Asasi za Kiraia zielekezwe kwenye miradi ya kipaumbele ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Waziri ameandika hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter akieleza kikao alichofanya kwa njia ya mtandao na Mkurugenzi wa Shirika hilo, Kate Somvongsiri, akiwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Emmanuel Tutuba.

“Nimeiomba @USAID kuelekeza msaada wa Dola 1.3 bilioni sawa na zaidi ya Sh3 trilioni inazotaka kuipatia Tanzania kupitia Asasi za Kiraia, zielekezwe kwenye miradi ya kipaumbele ya Serikali ya Awamu ya Sita. Tutazisimamia vizuri,” ameandika Waziri Nchemba

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments