JAMII YATAKIWA KUWA NA UTAMADUNI WA KUFANYA MATENDO YA HURUMA




Jamii imetakiwa kuwa na Utamaduni wa kufanya Matendo ya huruma kwa watu wenye uhitaji katika jamii ili nao waweze pata tabasamu kupiti Matendo hayo ambayo waliya fanyiwa.

Wito huo Umetolewa Jijini Dar es salaam na Bi. Nyendo Kinyonga, Mtaalamu wa Elimu Mazingira na ulinzi wa Watoto Wakati akizingumza na Waandishi wahabari katika ya Maadhimisho Taasisi ya Tanzania Girl Guides association, na kuitumia siku hiyo kutoa msaada katika kituo cha Tumaini la Maisha Tanzania kinacho lea watoto wenye Ugojwa wa Saratani kilichopo Hospital ya Taifa Muhimbili.

Bi.Kinyonga Amesema kuwa Kila Mtu anawajibu wa Kushiriki na kufanya Matendo mema katika jamii hasa kwa Makundi maalumu ili kuhakikisha Usawa wa kijinsia yanapewa kipao na kufikia malengo endelevu ya milenium 2030 yaliyo wekwa na Ulimwengu

Ameongeza kuwa Kauli mbiu ya Madhimisho ya Mwaka huu ni Dunia yetu Mustakabali katika Maswala ya Usawa wa Kijinsia hivyo Kupitia kauli mbio Ina hamasaisha jamii jinsi kukabiliana na changamoto ya tabia ya nchi.

Naye Bi.Cecilia Shayo kamaishina wa Manispaa ya Kinondoni amesema kuwa jamii Ina wajibu wa kuwalinda watoto wakike ili kuhakikisha watoto hao Wanakuwa na makuzi mema na yenye kuwasaidia katika maisha yao ya badae.

Aidha Bi Shayo amseama kuwa katika kuadhimisha siku ya GirlGurld wanatumia siku hiyo kufanya Matendo ya huruma na kuwaandaa watoto hasa watoto wakike kuwana na hamasa na Moyo wa kujitoa katika jamii.

Na Dominic Haule

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments