JERRY MURO MKUU WA WILAYA YA IKUNGI ATAJA MAFANIKIO LUKUKI MWAKA MMOJA WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN MADARAKANI

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Jerry Muro akizungumza na Wananchi na Wana CCM wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya hiyo katika hafla ya Mwaka Mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan iliyofanyika jana Viwanja vya Hospitali hiyo  ambayo ujenzi wake unaelekea kukamilika hivi karibuni.

                      
                                                           #IkungiYetu #AfyaYetu #SSH
Katika kipindi cha mwaka mmoja Rais, Samia Suluhu Hassan ameidhinisha zaidi ya shilingi bilioni 12.4 katika sekta ya afya wilaya ya ikungi katika miradi mipya ya Ujenzi wa Hospitali, vituo vya afya na zahanati pamoja na mishahara ya watumishi sekta ya afya

Tumeidhinishiwa milioni 800 umaliziaji wa hospitali mpya ya wilaya ujenzi uko asilimia 80, tumeidhinishiwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vinne vipya vya afya Iyumbu fedha za umaliziaji, iglanson, ntuntu, na irisya

Pamoja na kuidhinishwa fedha hizo pia tumepokea fedha Milioni 200 ajili ya ujenzi wa zahanati mpya katika vijijini vinne pamoja na fedha za dawa na vifaa tiba na mishahara ya watumishi katika sekta ya afya

Muonekano wa baadhi ya majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Ikungi ambayo yalikaguliwa na Wananchi wakati wa maadhimisho ya Mwaka Mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa madarakani.
                                           
Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi Stamili Dendegu akizungumza kwenye hafla hiyo wakati akimkalibisha mgeni rasmi Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo Mika Likapakapa. (hayupo pichani)
                                            

Hafla ikiendelea. Kutoka kushoto ni ,Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Ally Rehani, Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Abubakar Muna na Mchungaji wa Kanisa la Wasabato (SDA) Wilaya ya Ikungi, Joseph Metarus.
                                              
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa akihutubia katika hafla hiyo.
                                                  

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments