MAYELE AENDELEA KUTETEMA, YANGA YAONDOKA NA ALAMA TATU MBELE YA GEITA GOLD


KLABU ya Yanga imeendelea kuusogelea ubingwa wa ligi ya NBC mara baada ya leo kuichapa Geita Gold 1-0 kwenye dimba la CCM Kirumba Jijini Mwanza.

Fiston Mayele ameendelea kuwatesa makipa wa ligi kuu ambapo leo tena kaweka kambani goli la pekee lililowapa pointi tatu muhimu kwenye ligi hiyo.

Mayele alifunga bao la mapema kabisa baada ya kuwashinda mabeki wa Geita Gold na kuweza kukwanjuka shuti kali lililomshinda kipa wa Geita Gold.

Mechi hii ambayo ilikumbwa na faulo nyingi kwa pande zote mbili na kusababisha wachezaji baadhi kutolewa nje kwa majeruhi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments