SERIKALI ITAENDELEZA MAZURI YOTE YA HAYATI DKT. JOHN POMBE MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia Wananchi wa Chato pamoja na Wageni kutoka Sehemu mbalimbali nchini katika Kumbukizi ya Mwaka mmoja tangu kufariki dunia kwa Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Misa Takatifu iliyofanyika katika uwanja wa Michezo wa Magufuli leo tarehe 17 Machi, 2022. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka Shada la Maua katika Kaburi la Aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Misa Takatifu iliyofanyika katika uwanja wa Michezo wa Magufuli leo tarehe 17 Machi, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha kumbukumbu kabla ya kuweka Shada la Maua katika Kaburi la Aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika Kumbukizi ya Mwaka mmoja tangu kufariki dunia kwa Hayati Dkt. Magufuli leo tarehe 17 Machi, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimfariji Mama Janeth Magufuli baada ya kuweka Shada la Maua katika Kaburi la Aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Misa Takatifu iliyofanyika katika uwanja wa Michezo wa Magufuli leo tarehe 17 Machi, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kuendeleza mazuri yote yaliyoachwa na Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na kuleta mema mengine mapya.

Rais Samia amesema hayo leo wakati wa maadhimisho ya kumbukizi ya mwaka mmoja ya kifo cha aliyekuwa Rais Hayati, Dkt. John Magufuli Wilayani Chato Mkoani Geita.

Mhe. Rais Samia amemwelezea Hayati Magufuli kuwa Kiongozi aliyepinga rushwa na ubadhirifu, na kusisitiza uchapakazi na uzalendo kwa Taifa.

Rais Samia amewaahidi wananchi wa Chato kuwa Serikali itakamilisha na kushiriki kuifungua miradi yote ya maendeleo ambayo imeshakamilika ikiwemo stendi mpya ya Chato, uwanja wa ndege wa Chato uliofikia asilimia 95 pamoja na kivuko cha Chato.

Vile vile, Rais Samia ametoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuelimishana na kuhamasishana kushiriki katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi litakayofanyika Agosti, 2022.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments