Waendesha bodaboda Lushoto watakiwa kujisajili

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Kalisti Lazaro akizungumza na baadhi ya waendesha bodaboda Wilayani humo. Picha na Raisa Said
Waendesha bodaboda wilayani Lushoto mkoani Tanga wametakiwa kusajili umoja wao ili waweze mikopo kutoka halmashauri na taasisi za fedha badala ya kujiingiza kwenye mikopo kandamizi ya mitaani.

Wito huo umetolewa leo Jumatano Machi 16, 2022 na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto (DC), Kalisti Lazaro alipokuwa akizindua Chama cha Bodaboda wilayani humo.

Amesema kuwa usajili wa chama utawapa uwezo wa kutumia fursa ya mikopo kutoka halmashauri na taasisi za fedha kama benki badala ya kuteseka na mikopo kandamizi.

Lazaro amezindua Chama cha Umoja wa Waendesha Pikipiki Wilaya ya Lushoto (Uwapilo) ambacho kina wanachama 4,200.

Awali, akisoma risala kwa niaba ya umoja huo, Katibu wa Uwapilo, Mwema Jacob alisema ukosefu wa mikopo kutoka Halmashauri na taasisi nyingine za fedha ni mojawapo ya changamoto kubwa inayowasababisha kutegemea kuajiriwa au kuingia katika mikataba kandamizi.

Jacob alisema kuwa walikuwa wanaingia mikataba kandamizi na wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa leseni za udereva na mafunzo ya usalama barabarani.

Waliomba vituo vya bodaboda na waendesha bodaboda kusajiliwa katika mfumo maalumu wa kanzi data wa Taifa na usajili huo uwasilishwe kwa mkurugenzi wa Halmashauri.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments