Dar yajipanga kupambana na ‘Panya Road’

Kufuatia matukio ya uporaji yanayofanywa na vijana wanaojulikana kwa jina la Panya Road jijini hapa, baadhi ya wakazi wameweka mikakati ya kupambana nao.

Juzi vijana hao walisababisha taharuki baada ya kuwajeruhi watu 23 na kuwapora fedha, simu na vifaa vya kielektroniki, zikiwemo televisheni katika maeneo ya Chanika na Tabata jijini hapa.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Jumanne Muliro akizungumza na waandishi wa habari juzi alisema wanawashikilia vijana 10 kuhusiana na tukio hilo, huku wakiendelea kuwatafuta wengine.

Akizungumza na Mwananchi jana Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng’wilabuzu Ludigija alisema tayari ameshatoa maelekezo kwa wenyeviti wa Serikali za mitaa isiyokuwa na vikundi shirikishi kuanzisha mara moja.

Ludigija alisema kuna mitaa imejisahau, hasa kwenye suala zima ulinzi shirikishi, jambo linalosababisha watu wasiokuwa waaminifu kufanya uhalifu.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments