RAIS SAMIA SULUHU AKUTANA NA KUZUNGUMZA MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI KAMALA HARRIS, IKULU YA MAREKANI JIJINI WASHINGTON

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Makamu wa Rais wa Marekani Mhe. Kamala Harris mara baada ya kuwasili Ofisini kwake katika Ikulu ya Marekani White House Washington leo tarehe 15 Aprili, 2022.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na Mwenyeji wake Makamu wa Rais wa Marekani Mhe. Kamala Harris wakati wakizungumza na Wanahabari katika Ikulu ya Marekani White House Washington leo tarehe 15 Aprili, 2022.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwenyeji wake Makamu wa Rais wa Marekani Mhe. Kamala Harris wakati akiangalia mandhari ya Majengo ya Ofisi za Ikulu ya Marekani mara baada ya kuzungumza na Wanahabari katika Ikulu hiyo ya White House Washington leo tarehe 15 Aprili, 2022.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mazungumzo Rasmi na Ujumbe wa Serikali ya Marekani ulioongozwa na Makamu wa Rais wa Marekani Mhe. Kamala Harris katika Ikulu ya White House Washington leo tarehe 15 Aprili, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiagana na Makamu wa Rais wa Marekani Mhe. Kamala Harris mara baada ya mazungumzo na Ujumbe wa Tanzania katika Ikulu ya Marekani Whitehouse nchini Marekani leo tarehe 15 Aprili, 2022. PICHA NA IKULU

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments