Hakainde Hichilema |
Wizara inayosimamia mshahara na posho za Rais wa Zambia imesema Hakainde Hichilema binafsi ameamua kutopokea mshahara wowote, na ameamua atangulize mbele maslahi ya wananchi kwa kuwahudumia.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Rais wa Zambia amesema mshahara hakikuwa kichocheo na sababu ya yeye kugombea nafasi hiyo, na anachotaka zaidi, ni kulihudumia taifa lake.
Aidha Hichilema, mchumi mwenye umri wa miaka 59 amekadhibisha ripoti zinazodai kuwa serikali haina nia ya kumlipa mshahara na kusisitiza kuwa: Sijaitilia maanani kadhia hiyo (yamshahara). Azma na motisha yangu ni kutazama namna tunavyoweza kuboresha maisha ya wananchi.
Hakainde Hichilema |
Hichilema ambaye alitangazwa kuwa mshindi katika uchaguzi wa rais uliofanyika Agosti mwaka uliopita, akimuangusha vibaya Rais Edgar Lungu wa chama tawala, alisema wakati huo kuwa amerithi 'hazina tupu', huku kukiwa na taarifa za kiasi kikubwa cha fedha kuibiwa katika hazina ya taifa ya nchi hiyo.
0 Comments