Ujenzi SGR Makutupora-Tabora Kukamilika Miezi 42

Magenge ya wabeba silaha Ituri
Hayo yameripotiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) ambayo imeongeza kuwa, raia 20 miongoni mwao waliuawa jana Jumatatu katika eneo hilo.

Taarifa ya OCHA imeeleza kuwa: Kwa akali raia 20 waliuawa mapema leo (jana Jumatatu Aprili 11) kufuatia shambulizi la wabeba silaha katika mji wa Mangusu, eneo Irumu. Washambuliaji walipora pia nyumba na maduka katika miji jirani ya Bavonkutu na Bandiboli.

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa limebainisha kuwa, mbali na watu 20 kuuawa jana, wengine zaidi ya 40 wameuawa ndani ya siku saba zilizopita katika eneo la Irumu mkoani Ituri, kaskazini mwa DRC.

Watu wasiopungua 60 wameuawa katika mashambulizi ya magenge ya wabeba silaha kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
OCHA imesema mashambulizi mabaya zaidi yalishuhudiwa tarehe 6, 8, na 10 katika mkoa huo, na kwamba mashirika ya misaada ya kibinadamu yamesimamisha shughuli zao katika maeneo hayo.

Ripoti mbalimbali za vyombo vya habari zinaarifu kuwa, watu zaidi ya milioni 1.9 katika mkoa wa Ituri wamelazimika kuwa wakimbizi mkoani Ituri, kutoka na hujuma hizo za magenge ya wabeba silaha.

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments