YANGA YAENDELEZA UBABE, YAICHAPA NAMUNGO FC NA KUJICHIMBIA KILELENI

 

YANGA imeendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya Kutwaa ubingwa wa 28 baada ya kuvunja mwiko wa kutokupata ushindi toka kwa Namungo FC baada ya kuichapa mabao 2-1 mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Yanga walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Fiston Mayele dakika ya 17 akipiga tobo mlinda mlango David Mapigano.

Shiza Kichuya aliisawazishia Namungo dakika ya 33 akifunga bao safi kwa shuti kali lililomshinda kipa wa Yanga Diarra Djigui bao la ushindi kwa Yanga limewekwa kimiani na Feisal Salum ‘Fei Toto’ dakika ya 38.

Kwa ushindi huo Yanga wamefikisha Pointi 54 na kuendelea kujichimbia kilele mwa msimamo wa Ligi hiyo huku wakituma salamu wa watani zao Simba ambao mechi yao dhidi ya watani utapigwa April 30,2022

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments