AZAM FC YAIKAZIA SIMBA SC, YALAZIMISHWA SARE 1-1


MABINGWA Watetezi Simba wameshindwa kutamba ugenini dhidi ya Azam FC baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa uwanja wa Chamazi Complex nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Azam FC walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za Simba katika dakika ya 17 bao likifungwa na Mshambuliajia Rodgers Kola,Mshambuliaji wa zamani wa Azam ,John Bocco aliisawazishia timu yake dakika ya 44.

Kipindi cha pili timu zote ziliafanya mabadiliko na kuanza kushambualiana kwa zamu hadi dakika 90 zinamalizika timu hizo zimeweze kugawa pointi moja moja.

Kwa Matokeo hayo Simba wamefikisha Pointi 50 wakizidiwa Pointi 10 na Vinara wa Ligi hiyo Yanga wenye Pointi 60 ,Timu zote zikiwa zimecheza mechi 24 na kubakiwa na mechi sita huku Azam FC wakibaki nafasi ya tano wakiwa na Pointi 33.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments