Agizo hilo limetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Greyson Msigwa wakati maofisa hao walipotembelea Bandari ya Tanga na kuona maendeleo ya upanuzi Gati la bandari hiyo pamoja na uongezaji wa kina cha bandari.
Amesema Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya bandari ambapo ameitaja maeneo inakotekelezwa miradi hiyo kuwa ni Tanga, Mtwara na Dar es Salaam.
Awali, akisoma taarifa ya maendeleo ya utekekezaji mradi wa upanuzi wa Gati la Bandari ya Tanga, Mhandisi Hamisi Kipalo amesema mpaka umefikia asilimia 45
" Mradi huu unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo kwa awamu ya kwanza ilikuwa ni kuongeza kina, na tumefikia asilimia 98 na hii ni awamu ya pili ni upanuzi wa Gati," amebainisha Mhandizi Hamisi.
Kwa upande wake Ofisa Habari Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Raya Suleimani amesema amepokea maelekezo ya Msemaji Mkuu wa Serikali na kwamba watayanyia kazi.
"Ni wajibu wetu kutangaza miradi na kazi zinazofanywa na serikali ili wananchi waweze kuwa na taarifa za namna Serikali yao inavyotekeleza miradi mikubwa," amesema Raya.
0 Comments