Mbunge Ataka Wabadhirifu Wa Maji Wachukulie Hatua

Mbunge wa Nanyumbu (CCM), Yahaya Mhata amemtaka Waziri wa Maji Jumaa Aweso kuchukua hatua kwa wabadhirifu wa miradi miwili ya maji kwenye jimbo lake.

 Mhata ameyasema hayo wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka 2022/2023.

Amesema kata ya Nandete wilayani Nanyumbu kulikuwa na mradi mkubwa wa maji ambao ulichezewa.

“Nilikuomba ulete wakaguzi, watu wamechakachua ule mradi, mradi umetumia fedha nyingi lakini hautoi maji ya kutosha. Hatutakubali fedha za Serikali za walipa kodi watu wachache wananufaika,” amesema.

Aidha, Mhata amesema katika kata ya Mnanje kuna mradi wa Benki ya Dunia (WB) ambao tangu umezinduliwa haujawahi kutoa hata ndoo moja ya maji.

“Naomba waliohusika na ule ubadhirifu wachukuliwe hatua. Hili jambo halikubaliki, muda wa kuchezea maji, wakuchezea fedha za miradi ya maji ndani ya wizara yako mbele yaw ewe (Waziri) muda umekwisha,”amesema.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments