Rais Samia akiambatana na viongozi waandamizi wa CCM na Serikali walikutana na ujumbe wa viongozi wa Chadema, ulioongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma na kufanya mazungumzo ambayo bado hayajawekwa wazi na pande hizo mbili.
Mazungumzo baina na Rais Samia na viongozi hao wa chama kikuu cha upinzani ni mwendelezo wa kiongozi huyo mkuu wa nchi wa kukutana na makundi mbalimbali ya wadau wa demokrasia ili kuleta utengamano wa Taifa.
Wasomi hao walieleza hayo jana kwa nyakati tofauti, wakati wakizungumza na Mwananchi na kuongeza kuwa hatua ya viongozi wa CCM kukaa meza moja na Chadema inaashiria huenda Taifa likashuhudia siasa safi kwa siku zijazo.
Mchambuzi wa masuala ya siasa, Dk Faraja Kristomus alisema kikao cha uongozi wa juu wa Chadema na CCM chini ya Rais Samia kinatoa picha mbili tofauti.
0 Comments