Mkutano wa CCM, Chadema waibua hisia tofauti

Siku moja baada ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wakiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuonana na ujumbe wa viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), baadhi ya wasomi wameeleza faida na hasara ya mkutano huo.

Rais Samia akiambatana na viongozi waandamizi wa CCM na Serikali walikutana na ujumbe wa viongozi wa Chadema, ulioongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma na kufanya mazungumzo ambayo bado hayajawekwa wazi na pande hizo mbili.

Mazungumzo baina na Rais Samia na viongozi hao wa chama kikuu cha upinzani ni mwendelezo wa kiongozi huyo mkuu wa nchi wa kukutana na makundi mbalimbali ya wadau wa demokrasia ili kuleta utengamano wa Taifa.

Wasomi hao walieleza hayo jana kwa nyakati tofauti, wakati wakizungumza na Mwananchi na kuongeza kuwa hatua ya viongozi wa CCM kukaa meza moja na Chadema inaashiria huenda Taifa likashuhudia siasa safi kwa siku zijazo.

Mchambuzi wa masuala ya siasa, Dk Faraja Kristomus alisema kikao cha uongozi wa juu wa Chadema na CCM chini ya Rais Samia kinatoa picha mbili tofauti.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments