Akizungumza hivi karibuni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha Mhandisi Herini Mhina katika semina ya siku moja ya kuwapa uelewa wakandarasi juu ya mfumo huo
Alisema kuwa kupitia mfumo huo wa kidijitali utakwenda kuondoa changamoto mbalimbali na za mda mrefu ambazo zilikuwa zikiwakabili wateja
"Kwa mfumo ulivyo utaongeza uwazi zaidi na kutatua kero za vishoka ambao walikuwa wakisumbua wateja na kusababisha hasara kubwa "Alisema Mhandisi Mhina
Aliongeza kuwa kwa namna mfumo unafanya kazi utakwenda kumrahisishia mteja kufanya huduma akiwa nyumban kwa tumia simu ya mkononi
Kwa upande wake meneja wa EWURA Lorivil Longidu alipongeza shirika hilo kwa kuja na ubunifu mkubwa wa kuanzisha mfumo huo ambao utakaokwenda kutatua changamoto za wateja
Alisema kuwa kazi zote za ufundi wa umeme zitafanywa na wakandarasi au watu wenye leseni za EWURA
Na Pamela Mollel,Arusha
0 Comments