Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (Tucta) limemkumbusha Rais Samia Suluhu Hassan ahadi yake ya kuboresha mishahara kwa wafanyakazi na kupendekeza kima cha chini cha mshahara kwa sekta zote kiwe Sh1, 010,000 milioni.
Katibu Mkuu wa Tucta, Henry Mkunda ameyasema hayo leo Jumapili Mei Mosi, 2022 wakati akizungumza katika sherehe za siku ya wafanyakazi duniani inayofanyika katika uwanja wa Jamuhuri jijini hapa.
“Tunakumbuka ahadi yako ya kuboresha mishahara katika mwaka huu wa 2022, hivyo Tucta tunapendekeza kiwango cha kumwezesha mfanyakazi kuishi kiwe walau Sh1, 010,000 kwa mwezi baada ya hizi tafiti kufanyika. Tutashukuru sana Mama kama utaliona hilo,”amesema.
Mkunda amesema sababu iliyowasukuma kuandaa kauli mbiu ya Mei Mosi ya mishahara na maslahi kwa wafanyakazi ndio kilio chetu, Kazi iendelee ni wafanyakazi kuwa raslimali na nyenzo ya kuinua uchumi katika nchi.
0 Comments