UTAPENDA MANENO YA MADAME RITA KWA RAIS SAMIA BAADA YA KUIONA FILAMU YA THE ROYAL TOUR

MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Benchmark Productions,Rita Paulsen maarufu kwa jina la Madame Rita amesema filamu ya The Royal Tour imetengenezwa kwa ustadi mkubwa na jambo ambalo amevutiwa nalo ni namna ambavyo Rais Samia Suluhu Hassan ambavyo ameuvaa uhusika.

Akizungumza na Michuzi TV saa chache kabla ya Rais Samia Suluhu Hassan kuizindua filamu ya The Royal Tour jijini Dar es Salaam ,Madame Rita amesema anampongeza Rais Samia Samia kwa kuuvaa uhusika na kushiriki katika filamu ambayo haijawahi kufanywa hapa nchini Tanzania.

“Kwa hiyo hii filamu italeta hamasa kubwa sana kwasababu Rais aliigiza vizuri , alivaa vizuri , kulikuwa na uhalisia sana, nampongeza Rais wetu.Nimeona, vipande vichache lakini nachoweza kusema imetengezwa kwa ustadi mkubwa sana.”

Madame Rita ambaye kwa miaka kadhaa sasa kupitia kampuni yake amekuwa akiibua vipaji vya wasanii wa muziki, amesema filamu ya RoyalTour imethibitisha kwa vitendo wanawake wanaouthubutu wa kufanya mambo makubwa kwa ajili ya Taifa lao.”Rais Samia amethibitisha kuwa wanawake wanaweza hata yale ambayo wengine wanaamini hayawezekani.Ameonesha uthubutu na uzalendo mkubwa kwa nchi yetu.”


 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments