UTATUZI WA MIGOGORO YA ARDHI KATA YA PUMA NA DUNG'UNYI* IKUNGI.

Mkuu wa wilaya ya Ikungi Ndugu Jerry C. Muro leo Tarehe 26/05/2022 ameanza kazi ya utatuzi wa mgogoro wa Ardhi baina ya kata mbili za Dung'unyi na Puma katika eneo la vijiji vya Wibia na Dung'unyi katika mbuga ya Njori

Dc Muro akiambatana na kamati ya usalama ya wilaya amekutana na na viongozi wa pande zote mbili pamoja na familia za wananchi wanaovutana katika eneo hilo hatua ambayo imeanza kuhatarisha amani na usalama wa mbuga hiyo inayotumiwa kwa kilimo na mifugo

Wakitoa taarifa za awali mwenyekiti wa kijiji cha Wibia Daniel Benedict Amasi na Alex Mateo Jingu wa kijiji cha Dung'unyi wamesema mgogoro huo ambao umeanzia katika familia mbili umeanza kuchukua sura ya mgogoro wa vijiji kutokana na utata wa mipaka inayotengeneza vijiji vyao

Katika hatua ya awali ya usikilizaji wa mgogoro huo ofisi ya mkuu wa wilaya imeanza kusikiliza pande zote za uongozi wa vijiji, familia zinazopingana uku ikizingatia maelekezo ya mkuu wa wilaya aliekuwepo wakati wa mapigano katika eneo hilo Mhe. Miraji Mtaturu pamoja na kuzingatia hukumu za mabaraza ya ardhi zilizopo


Imetolewa na ofisi ya mkuu wa wilaya ikungi 26/05/2022
 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments