IKUNGI KULINDA MTOTO

Mkuu wa wilaya ya Ikungi Ndugu Jerry C. Muro amewaongoza watoto katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Africa katika viwanja vya shule ya msingi Puma

Akizungumza katika maadhimisho haya Dc Muro amesema Ikungi tutamlinda mtoto na kutengenezea mazingira wezeshi na bora ya kupata haki zake za Msingi

Amewataka wazazi kutumia muda na familia zao haswa watoto katika kuhakikisha wanawalinda dhidi ya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa na kusisitiza jukumu la kulinda mtoto ni la kila mzazi

"Tuimarishe ulinzi wa mtoto, tokomeza ukatili dhidi yake. Jiandae kuhesabiwa."

Imetolewa ofisi ya mkuu wilaya ikungi
 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments