Kabaka akemea makundi wanawake CCM

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Gaudensia Kabaka amekemea makundi ndani ya chama hicho na kutaka kudumishwa kwa umoja na mshikamano ili kutengeneza timu moja ya ushindi kuelekea uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025.

Kabaka ametoa rai hiyo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, wakati akizungumza na wanachama wa chama hicho, ambapo amesema wanapaswa kuwa wamoja na kuepuka makundi.

 "Niwatake muwe na umoja na kusiwe  na makundi, wanawake tukigawanyika tukiwa na makundi, nchi nzima itakuwa na makundi, chama kitakuwa na makundi, na jeshi lenye makundi haliwezi kushinda," amesema.

Mwenyekiti huyo pia amekagua na kuweka jiwe la msingi katika nyumba ya Katibu wa UWT Mkia wa Kilimanjaro na wilaya ya Moshi Mjini, ambapo ameahidi kuchangia Sh4 milioni, katika katika ujenzi wa nyumba hizo ambazo zitagharimu Sh150 milioni hadi kukamilika.

Katibu wa chama cha mapinduzi Mkoa wa kilimanjaro, Jonathan Mabihya amesema chama kitahakikisha kinadhibiti na kuchukua hatua kwa wapanga safu wote katika kipindi hiki cha uchaguzi ndani ya chama.

"Hatutasita kuchukua hatua kwa wale wote wanaopanga safu na wale wote wanaokiuka taratibu za uchaguzi wa chama na jumuiya zetu," amesema mabihya.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments