Chama Cha Mapinduzi(CCM) kupitia Katibu Mkuu wake Daniel Chongolo kimekemea tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikalib kuwapangia watumishi wapya vituo vya kazi kwa upendeleo.
Akizungumza leo Juni 3, 2022 baada ya kupokea taarifa ya upungufu wa watumishi wa afya na Elimu katika baadhi ya vituo vya afya na Shule wilayani Busega Chongolo ametumia nafasi hiyo kueleza ni vema tabia ya kupeleka watumishi wapya kwenye vituo vya kazi kwa upendeleo ikaachwa na kila mtu anawajibu wa kufanya kazi popote.
Amesema kwamba wananchi katika mahali walipo wanahitaji kuhudumiwa.”Acheni urasimu wapelekeni watumishi wapya kwenye vituo vya kazi vyenye uhitaji acheni kuwarundika Sehemu moja" amesisitiza Chongolo.
Chongolo yupo Wilayani Busega mkoani Simiyu katika muendelezo wa ziara ya kikazi inayolenga kukagua Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo akizungumza leo Juni 3, 2022 baada ya kupokea taarifa ya upungufu wa watumishi wa afya na Elimu katika baadhi ya vituo vya afya na Shule wilayani Busega
Ndugu Chongolo anaendelea na ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Simiyu ambapo pamoja na mambo mengine ni kuimarisha na kuhimiza uhai wa chama kuanzia ngazi ya mashina.
Chongolo ambaye ameambatana na Mjumbe wa Kamati Kuu na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ngemela Lubinga atazungumza na wanachama wa Chama hicho pamoja na kukagua miradi ya maendeleo kama ilivyoahidiwa kwenye Ilani ya uchgauzi Mkuu mwaka 2020-2025.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akikagua ujenzi wa kituo Cha Afya Cha Mkula wilayani Busega huku akipata maelezo kutoka Kwa Mganga mkuu wa wilaya ya hiyo Dk.Godfrey Mbagali wakati akiendelea na ziara yake wilayani Busega mkoani Simiyu.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akiendelelea kukagua toka kukagua kituo cha afya Mkula wilayani Busega.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akitoka kukagua kituo cha afya Mkula wilayani Busega.
Baadhi ya Madarasa yaliyojengwa kwa fedha za UVIKO
0 Comments