MAPINDUZI YA KILIMO IKUNGI


Mkuu wa wilaya ya Ikungi Ndugu Jerry C. Muro ambae ni mwenyekiti wa kamati ya mazao ya wilaya amewashukuru wadau wa maendeleo walioshirikiana na serikali katika kufanikisha ujenzi wa ghala la kisasa la mazao katika kata ya sepuka kijiji cha mnang'ana lenye thamani ya milioni 248

Dc Muro amesema ghala linauwezo wa kuhifadhi gunia 5,000 za alizeti sawa na tani 300 ambapo pia ghala limejengwa likiwa na vyumba vitatu vya kisasa ofisi ya chama cha ushirika, ukumbi wa mikutano ukiwa na vifaa vya kisasa vya kutolea mafunzo kwa wakulima pamoja na chumba cha kuhifadhia pembejeo za kilimo

Kukamilika kwa Ghala hili sasa kutaongeza thamani ya alizeti ambayo itatunzwa vizuri na kuuzwa katika bei ambayo itamsaidia mkulima kupata faida zaidi uku chama cha ushirika kikiwa na uwezo wa kuwahudumia wakulima wengi wanaolima alizeti katika tarafa nzima ya sepuka

Tayari Ghala limeanza kupokea mazao ya alizeti ambayo yameanza kuvunwa katika msimu huu wa kilimo, uku Dc Muro akiwashukuru wadau wa maendeleo kutoka KOICA, UNFPA, UNWOMEN, FARM AFRICA NA KIWOHEDE




                           

Imetolewa na ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Ikungi

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments