Sh15.8 Trilioni Kugharamia Miradi Ya Maendeleo

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amesema inakadiriwa kuwa jumla ya Sh15.8 trilioni sawa na asilimia 36.2 ya Bajeti yote ya Serikali zitatumika kugharamia miradi ya maendeleo ikijumuisha miradi ya huduma za jamii kwa mwaka 2022/23.

Dk Nchemba amesema hayo leo Jumanne Juni 14, 2022 wakati akiwasilisha hali ya uchumi wa Taifa na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka wa fedha 2022/23.

“Kati ya kiasi hicho, Sh12.8 trilioni sawa na asilimia 82.0 ya bajeti ya maendeleo ni fedha za ndani na Sh2.1 trilioni sawa na asilimia 18.0 ya bajeti ya maendeleo ni fedha za nje.” Amesema Dk Mwigulu

Amesema katika kuongeza ushiriki wa sekta binafsi kama injini muhimu ya utekelezaji wa miradi, Serikali itahakikisha miradi yote inayovutia uwekezaji wa sekta binafsi inatekelezwa kwa utaratibu wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) na Joint Venture kwa kutumia utaratibu wa Kampuni Maalumu (Special Purpose Vehicle).

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments