Shule Kufunguliwa Agosti 15

Wizara ya Elimu nchini Kenya, imesogeza mbele muda wa kufunguliwa kwa shule hizo kutoka Agosti 11, 2022 iliyotangaza awali hadi Agosti 15 ili kupisha ukamilishwaji wa mchakato wa uchaguzi mkuu uliofanyika jana, Jumanne Agosti 9, 2022.

Uamuzi huo umetangazwa leo, Waziri wa Elimu, George Magoha baada ya kuwapo kwa mijadala juu ya shule hizo kufunguliwa kesho wakati mpaka saba bado shughuli hiyo inaendelea huku baadhi ya maeneo wakazi wake hawajapiga kura.

Fuatilia matokeo uchaguzi mkuu Kenya hapa


Baadhi ya walimu, wazazi, walezi na wanafunzi walipinga uamuzi wa awali wa wizara hiyo kufungua shule Agosti 11 baada ya kuzifunga Agosti 5 kwakuwa shule hizo ndizo zinazotumika kama vituo vya kupigia na kuhesabu kura hivyo walihitaji muda zaidi wa wanafunzi kusalia nyumbani.
Hata hivyo leo, Waziri Magoha ameeleza "Baada ya mashauriano, natangaza uamuzi wa Serikali kwamba taasisi za elimu ya msingi zitafunguliwa kuanzia Jumatatu (Agosti 15, 2022)”.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments