Singida Manispaa Mshindi Wa Jumla Katika Mashindano (UMISETA)Singida.

Ushirikiano  Baina ya walimu wa michezo, wakuu wa shule na maafisa elimu, Michezo Na Vyama Vya Michezo  umeiwezesha Halmashauri ya Manispaa Ya Singida  kuibuka mshindi wa jumla katika mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) Ngazi ya Mkoa wa Singida  Ikizoa vikombe Vinne  vya mshindi wa kwanza katika michezo mbalimbali.

 Kauli hiyo ilitolewa Na Afisa Elimu   Mkoani Singida  Maria Lyimo,  alipokua akiongelea siri ya mafanikio ya Michezo Mkoani  Singida   katika kilele cha michezo ya UMISETA ngazi ya Mkoa iliyofanyika Katika viwanja vya shule ya sekondari Mwenge.

 Afisa Elimu Mkoa Wa Singida Maria Lyimo Limo  alisema “Mkoa Wa Singida tumejipanga vizuri. Mara tu baada ya kumaliza Mashindano ya mwaka jana. Tulianza mikakati mapema kuanzia ngazi ya shule, tarafa na wilaya”.

 Mkuu huyo wa Idara ya Elimu Sekondari alisema kuwa ushirikiano mkubwa baina ya walimu wa michezo, wakuu wa shule na maafisa  Kwa Kupitia Mwenyekiti Wa Chama Cha Mpira Wa Miguu Na Mwenyekiti Wa Kamati Ya Michezo Mkoa Wa Singida Bw Hamis Kitila ndiyo siri kubwa ya mafanikio kwa timu ya (UMISETA) ya Mkoa Wa Singida  kufanya vizuri. “Wakati wa kufanya uchaguzi wa wanamichezo Tulikuwa Na umakini mkubwa. Tuliwachagua kwa uwezo wao na siyo kwa upendeleo. Tuliwatumia Waamuzi wa Nje wenye sifa kuchezesha na kufanya uchaguzi makini wa wanamichezo kwa lengo la Kujenga timu Imara na itakayotoa ushindani na kulinda hadhi ya Mkoa Wa Singida.

 Kwa Upande Wa Mwenyekiti Wa Kamati Ya Michezo Mkoa Wa Singida Bw. Hamisi Kitila alisema kuwa Mkoa wa Wa Singida  una imani kubwa na timu hiyo ya mkoa. “Sisi viongozi wa mkoa hatuna maneno Mengi ya kusema, mengi mmeshaambiwa na viongozi wenu. Zingatieni taratibu za michezo hii, kwa jinsi Nilivyowaona hapa nidhamu imetamalaki. Mkoa tunawatakia ushindi mkubwa, mlete.

 Afisa Michezo Mkoa Wa Singida  Mwalim Amani Mwaipaja Amewashukulu Wadau Wote Walijitokeza Katika Kuwezesha Michezo Kufanyika Na Kumalizika Salama Kwa Ngazi Ya Mkoa Na Kupata Timu Ya Wanamichezo 120 Watakao Wakilisha Mkoa Katika Mashindano Ya (UMISETA) Kitaifa Yatakayofanyika Mkoani Tabora.

Tazama Picha Mbali Mbali Za Matukio Katika Ufungaji Wa Mashindano Ya (UMISETA) Nganzi Ya Mkoa Singida.

                              

























Na Abdul Bandola Ramadhani:Singida.
 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments