WAZIRI MKUU AFUNGUA KONGAMANO LA NNE LA KIMATAIFA LA NISHATI TANZANIA

 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Kongamano la Nne la Kimataifa la Nishati Tanzania kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere mkoani Dar es salaam, Agost 3, 2022.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama chombo kinachoonyesha ramani ya kiwanda cha kuchakata gesi asilia kinachotarajiwa kujengwa mkoani Lindi wakati alipotembelea banda la makampuni ya Shell na Equinor baada ya kufungua Kongamano la Nne la Kimataifa la Nishati Tanzania kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere mkoani Dar es salaam, Agost 3, 2022. Kulia ni Makamu wa Rais na Meneja wa Kampuni ya Uquinor nchini, Unni Merethe Fjaer na katikati ni Makamu wa Rais na Mwenyekiti wa Kampuni ya Shell nchini, Jared Kuehi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nishati, January Makamba katika Kongamano la Nne la Kimataifa la Nishati Tanzania alilolifungua kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere mkoani Dar es salaam, Agost 3, 2022
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Nne la Kimataifa la Nishati Tanzania wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua kongamano hilo kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere mkoani Dar es salaam, Agost 3, 2022.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments