YANGA SC BINGWA KWA MARA NYINGINE NGAO YA JAMII

 


MABINGWA wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara Timu ya Yanga imepindua meza baada ya kuongozwa bao mpaka kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya watani zao Simba mchezo wa Ngao ya Jamii ya kuashiria kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu mechi iliyopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

Simba walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 15 likifungwa na Kiungo Mshambuliaji Pape Sakho akipokea pasi Clatous Chama hadi mapumziko Simba walienda wakiwa wako mbele ya bao moja.

Kipindi cha pili Yanga walifanya mabadiliko kwa kuwaingiza Bernard Morrison na Jesus Moloko mnamo dakika ya 49 Mshambuliaji hatari Fiston Mayele,aliisawazishia Ysnga akipokea pasi ya Khalid Aucho

Mayele tena alirudi nyavu mnamo dakika ya 80 baada ya kupokea pasi ya Dickson Job na kuwanyanyua mashabiki wa Yanga.

Kwa ushindi huo Mayele ameipatia taji la kwanza la Ngao ya Jamii msimu wa 2022/23 baada ya mwaka jana kufunga bao moja na kuipa taji tena

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments