Ujenzi Wa Viwanja Vya Michezo Ni Jukumu La Serikali Na Wadau - Naibu Waziri Gekul

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul amesema ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya michezo ni jukumu la Serikali Kuu, Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Taasisi , Mashirika ya Umma na Wadau wa michezo.


Amesema hayo leo Septemba 16, Bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali wa Mhe. Shaban Omari Shekilindi (Lushoto) aliyeuliza Je ni lini Serikali itajenga Uwanja wa Michezo katika Mji wa Lushoto.

Napenda kutumia nafasi hii, kuzikumbusha Halmashauri nchini ikiwemo Halmashauri ya Lushoto, kuzingatia matakwa ya Sera ya Michezo kwa kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kukarabati na kujenga miundombinu ya michezo" amesema Mhe.Gekul.

Mhe.Gekul ameeleza kuwa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Mwaka 1995 ibara 7 inaeleza jukumu la ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya michezo ni jukumu la watu wote na mazingira ya kuwekeza yameainishwa kwa uwazi



TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments