Magaidi Wadaiwa Kuteketeza Shule

Magaidi wa Tehrik-e Taliban Pakistan (TTP) na wawezeshaji wao wameteketeza Shule ya Msingi ya Wasichana huko Samigal, Darel katika Wilaya ya Diamer ya Gilgit Baltistan (GB), vyombo vya habari vimeripoti.

Magaidi wa Tehrik-e Taliban Pakistan (TTP) na wawezeshaji wao wameteketeza Shule ya Msingi ya Wasichana huko Samigal, Darel katika Wilaya ya Diamer ya Gilgit Baltistan (GB), vyombo vya habari vimeripoti.

Idadi ya watu wa Samigal Pain ni karibu 7000 na ilikuwa shule pekee ya wasichana idadi yao ikifika 68 na hadi sasa hakuna kundi linalodai kuhusika.

Imeelezwa kuwa kuna kundi linapinga wasichana hao kupata fursa ya kupata elimu huko Gilgit Baltistan.


Tukio la wiki hii sio tukio la kwanza  kwa shule kuchomwa moto kwani mwaka 2018, shule 12 ziliteketezwa na kuwa majivu kwa usiku mmoja.

Matukio kama hayo yalitokea pia mwaka  2005 na  The Diamer Youth Movement (DYM) ilifanya maandamano huko Siddique Akbar Chowk, Chilas ambapo watu wa kada mbalimbali walilaani vikali kuchomwa kwa shule na kuimba kauli mbiu dhidi ya Serikali ya Gilgit Baltistan.

Vyombo vya habari viliripoti kwamba wazungumzaji waliwataka watu kukataa uhusiano na magaidi na kubainisha kuwa hawana matumaini kuhusu hatua ya serikali dhidi ya magaidi.

Rais wa DYM,  Shabbir Ahmed Qureshi na viongozi wengine walitaka hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya magaidi waliohusika katika tukio hilo wakitaka kukomeshwa kwa ubaguzi, kuwalinda watu wenye msimamo mkali.

Mwanaharakati wa haki za binadamu na mwanahabari Roshan Din Diameri alizungumzia tukio hilo na kusema daima kumekuwa na masuala mazito kuhusu elimu ya wasichana katika eneo hilo.

Kwa sasa wakazi wa wilaya ya Diamer wakazi wake asilimia 51 ni wanawake na wasichana wadogo ambao sasa wanajipanga kwa ajili ya kupata elimu.

Watu wa eneo hilo walikuwa wamekabiliwa na matatizo makubwa ya kuanza madarasa ya wasichana katika shule ya Samigal.

Watu wa Diamer walisema kuwa nia ya kundi hilo kutaka kuweka udhibiti kamili ni mojawapo ya sababu kuu za kuchomwa moto kwa shule hiyo.

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments