MWENYEKITI WA CCM RAIS SAMIA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA (10) WA UWT TAIFA JIJINI DODOMA

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Chama pamoja na Serikali wakati akiwasili kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma kwa ajili ya kufungua Mkutano wa 10 wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) tarehe 28 Novemba, 2022.



Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Viongozi mbalimbali wa Chama pamoja na Wanachama wakiimba nyimbo za CCM mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma kwa ajili ya kufungua Mkutano wa 10 wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) tarehe 28 Novemba, 2022. 

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi, wageni mbalimbali pamoja Wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kabla ya kufungua Mkutano wa 10 wa Jumuiya hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 28 Novemba, 2022.

Bendi ya Tanzania One Theatre (TOT) ikitumbuiza kwenye Mkutano wa 10 wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) uliofanyika kwenye katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 28 Novemba, 2022. 
Viongozi, wageni mbalimbali kutoka ndani na Nje ya Nchi pamoja Wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakiwa kwenye Mkutano wa 10 wa Jumuiya hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 28 Novemba, 2022.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments