SIMBA SC YAISHUSHIA KIPIGO CHA MABAO 3-1 POLISI TANZANIA

KLABU ya Simba imefanikiwa kuonoka na alama tatu mbele ya timu ya Polisi Tanzania baada ya kuichapa mabao 3-1 kwenye mchezo huo ambao ulichezwa kwenye dimba la Ushirika mjini Moshi.

Kwenye mechi hiyo tumeshuhudia mshambuliaji wao Moses Phiri akiweka kambani mabao mawili na kumfanya awe na mabao nane kwenye ligi kuu NBC na kuwa nafasi ya pili kwenye ufungaji mabao huku akiongza Fiston Kalala Mayele ambaye anamabao kumi.

Simba Sc ilianza kupata bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao John Bocco ambaye kwasasa amekuwa kwenye kiwango kizuri katika mechi tatu za hivi karibunu alivyoanza kupata nafasi kwenye kikosi.

Bao pekee la Polisi Tanzania limefungwa na Zuberi Khamisi dakika za lala salama

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments