TUNISIA HALI TETE KOMBE LA DUNIA

Timu ya taifa ya Tunisia imepoteza mchezo wake wa mzunguko wa pili wa Kundi D baada ya kufungwa bao 1-0 na timu ya taifa ya Australia katika mchezo wa Michuano ya Kombe la Dunia uliopigwa kwenye dimba la Al Janoub nchini Qatar.

Katika mchezo huo bao la Australia lilifungwa na Mitchell Duke kwenye dakika ya 23 ya mchezo huo, Wawakilishi wa bara la Afrika, Tunisia wamepoteza mchezo huo huku walifanikiwa kupata sare ya 0-0 dhidi ya Denmark huku Australia wakipoteza mabao 4-1 mbele ya Ufaransa.

Hali ni tete kwa Tunisia baada ya kuwa nafasi ya mwisho katika msimamo wa Kundi hilo wakiwa na alama moja pekee katika michezo miwili, huku Ufaransa wakiongoza msimamo wakiwa na alama tatu katika mzunguko mmoja.

Australia wakiwa na mizunguko miwili na nafasi ya tatu katika msimamo, wana alama tatu wakati Denmark wana alama moja wakiwa na mzunguko mmoja pekee, mchezo wa mzunguko wa tatu Tunisia atacheza na Ufaransa mchezo uliotajwa kuwa mgumu kwa Wawakilishi hao wa bara la Afrika.


 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments