ZIARA YA RAIS SAMIA MANYARA, KENANI AWAITA VIJANA WOTE KWENYE MAPOKEZI

Vijana mkoani Manyara wametakiwa kujitokeza kwa wingi kumpokea Rais Samia Suluhu Hassan anayetarajiwa kufanya ziara ya siku mbili mkoani hapa.


Wito huo ameutoa Katibu mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kenani Kihongosi wakati akizungumza na vijana wa Chama hicho mjini Babati ikiwa ni maandalizi ya ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan Novemba 22 na 23 mkoani Manyara.

Kenani amesema amefika katika mkoa wa Manyara kwa ajili ya ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuungana na vijana na kuwahamasisha kupitia Kauli mbiu yao isemayo 'Alipo Mama, Vijana tupo".

Amesema vijana lazima wamtie moyo Rais na kumuheshimisha kupitia mapokezi yatakayofanyika.

"Lazima mapokezi ya Rais katika mkoa wa Manyara yawe ya kipekee tofauti na mikoa mingine ambayo ameshakwenda" alisema Kenani.

Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Manyara Inyasi Amsi amesema Ugeni ni wa kwao Manyara na ni vijana hawana budi kujitokeza kuhamasishana kumlaki Rais.



TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments