IKUNGI NA UJENZI WA VYUMBA VIPYA 29 VYA MADARASA

Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mheshimiwa Jerry C. Muro leo tarehe 14/12/2022 amefanya ziara ya ukaguzi na kupokea taarifa ya ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa 29 katika shule 16 za majimbo ya singida mashariki na singida magharibi ujenzi ambao umegharimu shilingi milioni 580

Mhe. Muro akiwa pamoja na mhandisi wa halmashauri Millinga na afisa elimu sekondari Mwalimu Ngwano wametembelea shule zote 16 na kujiridhisha na kazi inayoendelea ya ujenzi ambapo mpaka kufikia leo ujenzi umeshakamilika kwa asilimia 99

Katika ziara hiyo Mhe. Muro pia amejionea zoezi la uwekaji wa viti na meza katika kila darasa kazi ambayo inaendelea kwa madarasa yote 29 na kusisitiza zoezi lazima liwe limekamilika mpaka kesho asubuhi tayari kwa ajili ya makabidhiano kwa Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Peter Serukamba siku ya alhamisi tarehe 15/12/2022










 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments