KAMATI YA MAWAZIRI 8 WA KISEKTA YAWASILI MKOANI KAGERA


Kamati ya Mawaziri Nane wa Kisekta imewasili rasmi mkoani Kagera kwa ajili ya kuongea na wakazi wa vijiji vinne vya kata ya Rutoro kuhusu uamuzi wa Baraza la Mawaziri juu ya vijiji hivyo ambavyo vimo ndani ya eneo la Ranchi ya Kagoma wilayani Muleba mkoa wa Kagera.

Kamati hiyo inaongozwa na mwenyekiti wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba ndaki na Makamu wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Ridhiwani Kikwete.

Wengine ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. David Silinde, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde, Naibu Waziri wa Maji Mhe. Eng. Maryprisca Mahundi, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Khamis Chilo.   

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments