Papa Benedict XVI Afariki DuniaAkiwa Na Miaka 95

Jumuiya ya wakristu wakatoloki duniani wamepata pigo baada ya kumpoteza aliyekuwa kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa Benedict XVI ambaye amefariki leo Jumamosi Desemba 31, 2022 katika makazi yake huko Vatican akiwa na umri wa miaka 95.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Papa ya Holy See Press, Benedict XVI amefariki katika makazi yake katika monasteri ya Mater Ecclesiae ambayo aliichagua kama makazi yake baada ya kujiuzulu mwaka 2013.

Wameeleza katika kipindi cha uhai wake Papa Benedict XVI aliongoza kanisa Katoliki kwa muda usiozidi miaka minane hadi, mwaka 2013, akawa Papa wa kwanza kujiuzulu tangu Gregory XII mwaka 1415.


Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Papa ya Holy See Press, Benedict XVI amefariki katika makazi yake katika monasteri ya Mater Ecclesiae ambayo aliichagua kama makazi yake baada ya kujiuzulu mwaka 2013.

Wameeleza katika kipindi cha uhai wake Papa Benedict XVI aliongoza kanisa Katoliki kwa muda usiozidi miaka minane hadi, mwaka 2013, akawa Papa wa kwanza kujiuzulu tangu Gregory XII mwaka 1415.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments