RAIS SAMIA ATEUA MAKATIBU WAKUU WA WIZARA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Jumatano Desemba 14, 2022 amefanya uteuzi wa makatibu wakuu wawili wa wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara (Uwekezaji) na Mambo ya Ndani.

Dkt. Samia amemteua Dk Hashil Twaibu Abdallah kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji ambaye awali alikuwa Naibu Katibu mkuu wizara hiyo kwenye upande wa Viwanda na Biashara nafasi ambayo iliyokuwa wazi.


Rais Samia amemteua Kaspar Mmuya kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ambaye awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu akishughulikia Sera, Bunge na Utaratibu.
Kabla ya Mmuya kuchukua nafasi hiyo, awali Katibu Mkuu wa wizara hiyo alikuwa Christopher Kadio

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments