Sababu Mwamposa kujaza Uwanja wa Mkapa Dar


 Dar es Salaam. Kama ulidhani mechi za watani wa jadi, Simba na Yanga ndizo pekee zinazojaza Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, utakuwa unajidanganya.

Baadhi ya makongamano ya dini yamethibitisha kuujaza uwanja huo hadi pomoni, hali ambayo wataalamu wa masuala ya kijamii wamesema watu wanajazana kwa sababu tano tofauti, wakiwemo wenye matatizo, wanaoamini na wanao kwenda kushuhudia na na kuhoji kinachofanyika.

Akizungumzia umati huo, mtaalamu wa saikolojia, Yisambi Mbuwi alisema watu waliokwenda katika mkesha ule wamegawanyika katika makundi tofauti, akisema miongoni mwao huenda wachache wakawa na hofu ya Mungu.


Mbuwi alisema kuna watu wamekwenda kwa kushawishiwa na marafiki zao au kufuata mkumbo, kusindikiza ndugu, wengine kwa kufuata miujiza au kumpeleka mgonjwa huku baadhi wamehudhuria kwa ajili ya kwenda kuangalia kinachofanyika na inawezekana miongoni mwao wakawa wapinzani wa Mwamposa.

“Kuna kundi limeenda kwa sababu linamwamini Mwamposa, wengine kwa sababu ya uhitaji kutokana na changamoto zinazowakabili, wengine ni wale waliokosa sehemu za kwenda wameamua kwenda ili kuonana na marafiki zao. Kundi jingine ni lile wanalokwenda kwa ajili ya ibada, kwa sababu Mwamposa yupo.

“Kisaikolojia maana yake ni mwitikio wa jamii, katika kundi la watu 10 wengine wanakuwa na mwitikio tofauti, hata kwenye miujiza baadhi wanakwenda wakiwa na sababu maalumu kama kupima imani ya mtumishi husika,” alisema Mbuwi.


Waujaza hadi nje

Juzi wafuasi wa Mtume Boniface Mwamposa waliujaza Uwanja wa Mkapa, wengine wakabaki nje.

Mwamposa, maarufu ‘Buldoza’ wa Kanisa la Arise and Shine (Inuka Uangaze), usiku wa kumkia jana aliendesha mkesha aliouita “Vuka na Chako Kabla ya Kuvuka Mwaka” ulioweka rekodi ya mahudhurio kwa kuujaza uwanja huo unaoweza kuchukua mashabiki 60,000 waliokaa, huku wengine wanaokadiriwa 20,000 wakikaa kwenye korido.


Mbuwi alisema kuna watu wamekwenda kwa kushawishiwa na marafiki zao au kufuata mkumbo, kusindikiza ndugu, wengine kwa kufuata miujiza au kumpeleka mgonjwa huku baadhi wamehudhuria kwa ajili ya kwenda kuangalia kinachofanyika na inawezekana miongoni mwao wakawa wapinzani wa Mwamposa.

“Kuna kundi limeenda kwa sababu linamwamini Mwamposa, wengine kwa sababu ya uhitaji kutokana na changamoto zinazowakabili, wengine ni wale waliokosa sehemu za kwenda wameamua kwenda ili kuonana na marafiki zao. Kundi jingine ni lile wanalokwenda kwa ajili ya ibada, kwa sababu Mwamposa yupo.

“Kisaikolojia maana yake ni mwitikio wa jamii, katika kundi la watu 10 wengine wanakuwa na mwitikio tofauti, hata kwenye miujiza baadhi wanakwenda wakiwa na sababu maalumu kama kupima imani ya mtumishi husika,” alisema Mbuwi.


Waujaza hadi nje

Juzi wafuasi wa Mtume Boniface Mwamposa waliujaza Uwanja wa Mkapa, wengine wakabaki nje.

Mwamposa, maarufu ‘Buldoza’ wa Kanisa la Arise and Shine (Inuka Uangaze), usiku wa kumkia jana aliendesha mkesha aliouita “Vuka na Chako Kabla ya Kuvuka Mwaka” ulioweka rekodi ya mahudhurio kwa kuujaza uwanja huo unaoweza kuchukua mashabiki 60,000 waliokaa, huku wengine wanaokadiriwa 20,000 wakikaa kwenye korido.


Kwa upande wake, John Joseph alisema Uwanja wa Mkapa ulifurika si kwa wakazi wa Dar es Salaam pekee, bali hata mikoa ya jirani ya Pwani na Morogoro walihudhuria mkesha huo.

Alisema kuanzia nje na ndani ya uwanja watu walikuwa wamejazana hadi kufikia juzi jioni.


Washinda uwanjani, wakesha

Watu walianza kuingia kwenye Uwanja wa Mkapa kuanzia juzi saa 12 asubuhi baada ya milango kufunguliwa.

Waumini waliotoka mikoani walikuwa wanaingia kwa kutumia milango ya D jirani na Uwanja wa Uhuru na wengine wakitumia mlango B jirani na ukuta wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (Duce).

Makundi tofauti yaliendelea kuingia uwanjani hapo na ilipofika saa nne asubuhi umati ulipoongezeka, maofisa usalama wa uwanja huo waliweka utaratibu wa ukaguzi.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments