YANGA SC YAONDOKA NA ALAMA TATU MBELE YA MTIBWA SUGAR

KLABU ya yanga immeweza kuondoka na alama tatu mbeleya Mtibwa Sugar baada ya kufanikiwa kuichapa bao 1-0, mchezo ambao ulipigwa katika dimba la Manungu mkoani Morogoro.

Katika mchezo huo Yanga Sc iliwakosa baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza lakini haikuwazuia kupata alama tatu kwenye mchezo wao huo muhimu ambapo Yanga alikuwa ugenini.

Bao pekee la Yanga Sc limewekwa kimyani na nyota wao Azizi Ki ambaye alipiga mpira wa adhabu ambao ulimshinda kipa wa Mtibwa Sugar Razaki na kutinga moja kwa moja wavuni na Yanga Sc kuondoka na ushindi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments