KIKWETE AIPONGEZA WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO KWA KUKUZA SANAA.



Rais mstaafu wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho ameipongeza Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo kutokana kufanya vizuri kwenye Sanaa ya Muziki na Sanaa ya Filamu hapa nchini.

Mhe. Kikwete amesema haya wakati akitoa hotuba yake usiku wa kuamkia leo Januari 29, 2023 kwenye ukumbi wa Mlimani City kwenye uzinduzi wa album ya the Kid you know ya msanii maarufu nchini Mario.

Amefafanua kuwa ili Sanaa iweze kukua hapa nchini inategemea mahitaji ya Serikali ambapo ametoa wito kwa Serikali kuendelea kulea sanaa

Amepongeza Wizara kwa kufanikisha kuwa na mdundo ambao utalitambulisha Taifa la Tanzania duniani.

Pia amepongeza kwa Serikali kuanzisha Mfuko wa Utamaduni na Sanaa na kuanza kutoa mikopo isiyo na riba na kuomba kuwa na mkakati madhubuti ambao utasaidia sanaa kwenye kwenye ngazi za kimataifa.

Tukio hili limehudhuriwa na mamia ya wapenzi wa muziki huku wasanii mbalimbali wa nyimbo za kizazi kipya wakimsindikiza Marioo katika uzinduzi wa album hiyo.

Pia Katibu Mkuu wa Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi na viongozi wengine pamoja na wadau mbalimbali wa muziki wamejitokeza    

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments