Recent-Post

Necta Yataja Sababu Ya Kutotangaza Wanafunzi, Shule Bora

Baraza la Mtihani la Taifa (NECTA), limetangaza sababu ya kutopanga na kutangaza shule na wanafunzi 10 bora waliofanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne, likisema limebaini hakuna tija ya kufanya hivyo.

Kauli hiyo imetolewa leo, Januari 29, 2023 na Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athumani Amasi wakati akitangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne kwa wanafunzi wa 2022.

"Ina tija gani kumtaja mmoja kati ya shule nyingi na tena bahati mbaya unamlinganisha mtu na mwingine ambaye hawakusoma kwenye mazingira yanayofanana,” amesema.



Post a Comment

0 Comments