Ajali hiyo imetokea leo Jumapili Februari 12, 2023 saa 9 mchana katika kijiji cha Mwibagi wilayani Butiama katika barabara ya Mwanza Musoma.
Mkuu wa wilaya ya Bunda, Dk Vicent Naano amesema kuwa majeruhi hao 20 wamekimbizwa katika hospitali hiyo na wanaendelea na matibabu.
"Tumepokea majeruhi 20 na watatu kati yao hali zao sio nzuri sana madaktari wanajitahidi kufanya kila wawezalo ili kuokoa maisha yao." amesema Dk Naano
Amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana kwa maelezo kuwa ajali hiyo imetokea wilaya ya Butiama.
"Wasiliana na watu wa Butiama sisi hapa tumepokea majeruhi tu taarifa za ajali bado hatuna, kwa sasa naweza kuongelea idadi ya watu waliolazwa hapa hospitalini." ameiambia Mwananchi kwa njia ya simu.
Endelea kufuatilia mitandao yetu kwa habari zaidi.
0 Comments