Hakuna Kutishwa Mtu Hapa, Asema Martha Mlata Mwenyekiti Wa CCM (M)Singida.

                
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata Amesema Hakuna Kutishwa mtu Hapa, Baada Ya Kumsikiliza mkuu Wa Mkoa Wa Singida Bw. Piter Serukamba Wakati Akituo Ripoti Ya Utekelezaji Wa Ilani Kwenye Kikao Cha Halmashauli Kuu Ya Mkoa Wa Singida Kilicho Fanyika Tarehe 19 Febury 2023. Mkoani Singida.              

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata akizungumza kwenye kikao hicho alipongeza ushirikiano uliopo baina ya watendaji wa Serikali na chama hicho na kwamba hata miradi iliyotembelewa na kamati ya siasa ya mkoa inakwenda vizuri.

Aidha Bi Martha  Mlata aliwataka wabunge kuacha kuwatishia wakuu wa wilaya na wakurugenzi na kwamba kunapokuwa na changamoto yoyote wafuate taratibu,

  Wakati huo  huo aliwaeleza wajumbe Wa Kikao hicho kuwa watendaji wanaletwa kwenye mkoa wetu ili watusaidie, kuleta maendeleo kwa faida yetu sasa na vizazi vijavyo tunatakiwa tuwape ushirikiano ili waweze kutekeleza majukumu yao vyema” alisema Mlata.


Kwa Upande Wa Mkuu Wa Mkoa Wa Singida Bw. Piter Serukamba amesema tunapaswa Kuache majungu na uongo ilikuendeleza umoja wetu kwakufanya kazi kwa bidii na kumuunga mkono kwa dhati Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania  Dr.Samia Suluhu Hassani Kwajili ya maeendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (  MNEC) Taifa Mkoa wa Singida, Yohana Msita, akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Katibu Mkuu wa CCM Mkoawa Singida, Lucy  Boniface akiongoza kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
Kikao kikiendelea. Kutoka kushoto ni Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Singida, Violet Soka, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Singida, Martha Ndungulu na Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Singida.Tatu Daghau.
Kikao kikiendelea.
Na Abdul Bandola Singida


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments