MNEC JUMAA AWAFARIJI WALIOTHIRIKA NA BOMOABOMOA MATUGA, KAWAWA

 Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (MNEC) kupitia Wazazi Hamoud Jumaa amefika kitongoji cha Matuga kata ya Kawawa,kuwafariji wahanga waliokumbwa na Zoezi la bomoabomoa ya makazi yao ambapo amewapatia vyakula.


Amewafariji wahanga kwa kuwapatia Unga, Sukari, Maharage, Pesa taslimu kwaajili ya vyoo vya dharura vya wanawake na wanaume.

Jumaa ameeleza ,anatambua wapo kwenye wakati mgumu na kuwaomba wahanga wawe na subira kwani Serikali na Chama Viko vinalifuatilia suala hilo kwa ukaribu na haki zitapatikana.

Amesema kwakuwa jambo hilo lipo katika mchakato wa kisheria ni vyema kuisubiria serikal itakuja na majibu sahihi.

Kitongoji cha Matuga kimekumbwa na bomoabomoa ya nyumba takriban 152 baada ya Maamuzi ya baraza la ardhi wilaya kuamuru eneo kurudi kwa mmiliki KADRI ambae wakazi hao na upande wa Zegereni kuvamia eneo la mmiliki huyo.




TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments